Wednesday, August 13, 2014

Mainda: Wasanii wengi maisha yao ni ya filamu



NA JENNIFER MANONI
RUTH Suka ni mwigizaji wa siku nyingi kutoka katika Kundi la Kaole Sanaa lililokuwa linatamba miaka ya nyuma na maigizo yake yaliyokuwa yanaonyeshwa kupitia televisheni ya ITV.
Mwanadada huyo ni miongoni mwa waigizaji wengi wanaofanya vizuri kwa sasa kwenye tasnia ya filamu Tanzania na Afrika Mashariki na Kati kwa ujumla.
Miongoni mwa waingizaji hao waliokuwa wanaunda kundi la Kaole wakati huo ni pamoja na Vicent Kigosi ‘Ray’, Hissan Muya ‘Tino’, Muhsin Awadh ‘Dr Cheni’ Elizabeth Michael ‘Lulu’, Marehemu Steven Kanumba, Blandina Chagula ‘Johari’ na wengine wengi.
Kupitia safu hii Dimba lilipata fursa ya kuzungumza na mwanadada huyo kwa ajili ya kujua mambo muhimu matano kutoka kwake ambayo yamekuwa ni sehemu ya mafanikio yake tangu alipoanza maisha yake ya filamu.
UPENDO
“Wasanii kwa sasa hatupendani hata kidogo hadi pale unapotokea msiba au sherehe ndiyo utawaona wakikaa pamoja na kujifanya wanampenda mtu ila wakati alipokuwa hai au alipokuwa na matatizo wanaishia kumsema pembeni tu, ila hii imenifanya kufanya kazi kwa bidii na kujitegemea badala ya kutegemea watu wengine.
CHANGAMOTO
“Changamoto kubwa katika kazi yangu ni wasanii wengi kutojali muda wa kufika kwenye eneo la kurekodia ‘location’ na mara kadhaa hii iankuwa nio tofauti na vile mnavyokubaliana. Mambo haya wakati mwngine najiuliza ni kwa nini mtu anafanya hivi au kuna nia ya kuniharibia kazi ila ndiyo hali ya watu ninaofanya nao kazi.
MAISHA YA WASANII
“Maisha ya wasanii ni mabaya ila wanalazimisha kuishi hivyo kwa kulazimisha kutokana na majina yao na ndiyo sababu wanajitahidi kubadilisha nguo na magari ambayo yanakuwa kitendawili kama ni ya kwao au wanayaazima. Kifupi maisha yao ni ya filamu au maigizo si maisha halisi.
MALENGO
“Kwa sasa nimesimama kwa muda naangalia kwanza soko la filamu linavyokwenda ili kama nitakuja kutoa filamu iwe na maana na siyo kulazimisha kutoa kazi nyingi zisizoeleweka. Kutokana na hilo naweza ukajikuta unauza jina badala ya kutafuta pesa kwa sanaa kwa sasa ni zaidi ya kazi na sio starehe peke yake na kuwafurahisha tu watu.
STAREHE
“Wasanii tumeweka starehe mbele kuliko kazi hiyo yote ni kutokana na kuridhika mapema kwa vijisenti anavyochukua au anavyopata kutokana na kazi husika, hili ni tatizo ambalo lazima sasa wasanii wenyewe wabadili fikra zao,” anasema nyota huyo.


No comments:

Post a Comment