Saturday, December 26, 2015

Waporaji wauawa Mbagala Kuu


VIJANA wa wawili katika eneo la Mbagala Mkuu wameuawa na wananchi wenye hasira badaa ya kupora beki la mwanamke mmoja mkazi wa Mbagala Kuu.
Tukio hilo lilitokea katika mtaa wa njia ya jeshini lafajiri ya leo ambapo baada ya kupora vijana hao waliokuwa watatu wakiwa na mapanga, bisibisi na vyembe walikimbia hadi mtaa wa makonde ambapo ndipo walipokamatwa na kisha kushambuliw ana wananchi wenye hasira wakiwa na silaha za jadi. 
katika tukio hilo mmoja ya vijana hao aliweza kukimbia na kufanikiwa kupona lakini mmoja alikimbilia kwenye moja ya choo kilichokuwa kwenye moja ya nyumba za mtaa huo ambapo wananchi hao walimfuata na kutoa kisha kupiga ambapo alimkata kata kisha kumuunganisha na mwenzake ambao waliwekwa kwenye eneo la wazi kisha kuchomwa moto.
Hata hivyo walikuonekana baadhi ya kina mama wakilia na wengine wakilaani tukio la kuuawa kwa vijana hao ambao hadi sasa bado hawajaweza kutambulika majina yao.
Katika siku za hivi karibuni eneo la Mbagala Kuu wameibuka vijana ambao wamekuwa wakifanya vitendo vya uporaji na uharibifu wa mali.
Desemba 24 mwaka huu mwanamke mmoja alipora kisha kubakwa na vijana ambao hawakufahamika mara moja wakati mwanamke huyo akitokea kazini majira ya saa 3:00 usiku.
Mbali na tukio hilo kumekuwepo na matukio ya kuvamiwa na kuporwa mali watu mbalimbali wakiwa kwenye mageti ya nyumba zao wakiwa wanasubiri kufunguliwa jambo lililozusha hasira kutoka kwa wananchi mbalimbali wa kato hiyo.

No comments:

Post a Comment