Wednesday, June 24, 2015

Muuaji wa Stars awaita Simba Taifa


NA MWANDISHI WETU
STRAIKA Mganda, Erisa Ssekisambu ambaye ndiye aliyeifunga mabao 2 kati ya 3 yaliyoitoa Taifa Stars katika mbio za  kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (Chan), amewataka matajiri wa Simba, kufika kwenye Uwanja wa taifa kushuhudia muziki wake.
Mganda huyo anayekipiga katika klabu ya SC Villa atakuwepo jijini Dar es Salaam akiambatana na timu yake inayokuja kucheza mechi ya tamasha maalum la kuzuia Mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino) Jumamosi katika Uwanja wa Taifa.
Ssekisambu amewaalika Simba baada ya kupata taarifa kwamba viongozi wa timu hiyo wameanza mbio za kusaka saini yake, ikiwa ni siku chache baada ya Shirikisho la soka nchini TFF kuridhia kuongeza idadi ya wachezaji wa kigeni kutoka watano hadi saba.
Akizungumza na toka nchini Uganda, Ssekisambu alisema endapo Simba watafika uwanjani na kuridhishwa na kiwango chake na pia watafikia makubaliano na viongozi wake basi hatokuwa na kikwazo cha kuvaa jezi nyekundu msimu huu na kuungana na Mganda mwenzake Emmanuel Okwi anayekipiga Simba.
Simba imo katika mawindo ya wachezaji watakaokiimarisha kikosi chake, ambapo juzi Rais wa klabu hiyo Evans Aveva alisema wanataka kufanya mapinduzi makubwa ya soka msimu huu kwa kusajili wachezaji wazuri na wenye uwezo watakaoirudishia ubingwa timu hiyo ya Msimbazi.
Msimu uliopita Simba haikufanya vizuri katika michuano ya Ligi Kuu ambapo licha ya kusajili nyota watano wa nje lakini ilishindwa kufurukuta na kujikuta ikimaliza ligi hiyo ikishika nafasi ya tatu.

usemavyo ubongo wa Kakore: Nooij alijifukuza kabla ya kufukuzwa




KOCHA wa Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ aliyefukuzwa, Mart Nooij, ni miongoni mwa watu waliopewa kipaumbele kwenye vyombo vya habari nchini Tanzania kwa muda wa wiki mbili ingawa kwa wiki iliyopita na mwanzoni mwa wiki hii nguvu hiyo iliongezeka.
Sababu za kupewa nafasi kubwa kwenye vyombo vya habari na midomoni mwa wapenzi na mashabiki wa soka la Tanzania, ni kutokana na Taifa Stars kufanya vibaya katika mechi tano mfululizo jambo ambalo halikuwa la kawaida kwa muda wote wa zaidi ya miaka 50 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kiukweli kocha huyu inawezekana alikuwa bora lakini kwa mwelekeo wa soka letu na mfumo wa soka letu alikuwa haendani nao, kwa kifupi ni kwamba, viatu alivyokuwa amevivaa vilikuwa havukumtosha.
Lakini jambo kubwa ambalo nililiona kwa Nooij, ni kukosa hamasa na ukaribu na wenye timu yao yaani Watanzania wenyewe, ndiyo sababu timu ilikosa hamasa  kama ilivyokuwa wakati wa Marcio Maximo na waliokuja baada yake; Jan Poulsen na Kim Poulsen.
Kosa hili lilikuwa wazi kwani Nooij alisahau kuwa Stars ni timu ya umma jambo lililomfanya kuiweka timu mbali na wenye timu, hili ndilo lilikuwa kosa la kwanza kwani hata alipokosea kidogo kwenye uwanja mashabiki hao walikuwa wa kwanza kumlaumu na kumkosoa.
Makosa ya aina hii hakuna kocha anayeweza kudumu kwenye timu za taifa kwani ninachofahamu mimi ni kwamba, moja ya sifa ya kocha wa timu ya taifa ni kuhakikisha inakuwa ni mali ya watu na si mali ya mtu.
Jambo lingine ni kushindwa kuwatumia makocha wazawa kwa ufasaha, hili limekuwa ni tatizo kubwa kwa makocha wengi wa kigeni wanaokuja kufanya kazi ingawa wale wanaowatumia wazawa wamekuwa wakifanikiwa.
Kwa mfano, Maximo aliweza kuwatumia makocha kama Juma Pondamali, Ally Bushiri, marehemu Sylverster Mash, ambao walikuwa wakilifahamu vyema soka la Tanzania kwani wamekuwa ni sehemu ya soka hilo.
Lakini angalia makocha waliokuja kwenye ngazi za klabu akiwemo Patrick Phiri alikuwa na wasaidizi wazawa akiwa na kikosi cha Simba na hata kocha wa sasa wa Yanga, Hans van der Pluijm pamoja na mafanikio yake ndani ya timu hiyo, amekuwa akitegemea uwepo wa makocha, Charles Mkwassa na kocha wa makipa, Juma Pondamali.
Mfumo huu ndio umewafanya makocha wengi duniani kufanikiwa, lakini ilikuwa kinyume kwa Nooij ambaye alikuwa akiamini katika kile anachokifahamu na naamini alikuwa hashauriwi vyema na wale waliokuwa wakimsaidia.
Hivyo kwa Nooij naye alitakiwa kuangalia mbali au kama wanavyosema vijana wa siku hizi alitakiwa kujiongeza zaidi na kuangalia mbali kwa kushirikisha katika kazi zake makocha wazalendo, lakini nasikitika kuwa pamoja na wingi wa makocha bora hawajatumika inavyostahili.
Hili limekuwa ni kosa ambalo limemgharimu Nooij na iwapo akija kocha mwingine kutoka nje ya Tanzania akipewa jukumu hilo kwa siku za baadaye lazima aambiwe ukweli wa jambo hili kwa maana akidharau atashindwa tena.
Lakini mwisho wa yote ni kwamba, lazima tukubaliane kuwa nchi yetu inahitaji kubadilisha mfumo wa soka na uendeshaji wake kwani bado tupo kwenye mfumo wa kizamani ambao hauwezi kutuvusha.
Miongoni mwake ni pamoja na kuimarisha soka la vijana na watoto kwani ndiko kwenye mtaji na maendeleo kwa soka letu na si jambo lingine lolote.
Hapa ndipo tulipokosea, lakini nikiangalia makocha wapo na wanaweza kutuvusha ila lazima tukubaliane kuwa hawa hawajatumika ipasavyo na kama likifanikiwa hili tunaweza kusogea mbele lakini si kwa aina ya kocha kama Nooij kutokana na msimamo wake na aina ya utendaji wake wa kazi.   
Kwa sababu hiyo, ninachokiona ni kwamba, Nooij alijifukuza kabla ya kufukuzwa kwenye kikosi cha timu ya taifa kwa kushindwa kuangalia alama za nyakati na wale waliomzunguka na kufanya naye kazi.

Saturday, June 20, 2015

hii ndiyo ratiba ya Ligi ya England


Agosti 8, 2015

Arsenal         v     West Ham       
Bournemouth    v     Aston Villa       
Chelsea         v     Swansea       
Everton        v     Watford       
Leicester        v    Sunderland       
Man United     v    Tottenham       
Newcastle Utd     v    Southampton       
Norwich        v    Crystal Palace       
Stoke City    v    Liverpool       
West Brom    v    Manchester City       

Agosti 15, 2015

Aston Villa    v    Man United       
Crystal Palace    v    Arsenal       
Liverpool        v    Bournemouth       
Man  City        v    Chelsea       
Southampton    v    Everton       
Sunderland    v    Norwich       
Swansea        v    Newcastle Utd       
Tottenham    v    Stoke City       
Watford        v    West Brom       
West Ham    v    Leicester       

Agosti, 22, 2015

Arsenal         v     Liverpool       
Crystal Palace    v    Aston Villa       
Everton        v    Man City       
Leicester         v    Tottenham       
Man United    v    Newcastle Utd       
Norwich        v    Stoke City       
Sunderland    v    Swansea       
Watford        v    Southampton       
West Brom    v    Chelsea       
West Ham    v    Bournemouth       

Agosti 29, 2015

Aston Villa    v    Sunderland       
Bournemouth    v    Leicester       
Chelsea        v    Crystal Palace       
Liverpool        v    West Ham       
Man City        v    Watford       
Newcastle Utd    v    Arsenal       
Southampton    v    Norwich       
Stoke City    v    West Brom       
Swansea        v    Man United       
Tottenham    v    Everton       

Septemba 12, 2015

Arsenal        v    Stoke City       
Crystal Palace    v    Man City       
Everton        v    Chelsea       
Leicester        v    Aston Villa       
Man United    v    Liverpool       
Norwich        v    Bournemouth       
Sunderland    v    Tottenham       
Watford        v    Swansea       
West Brom    v    Southampton       
West Ham    v    Newcastle Utd       

Septemba 19, 2015

Aston Villa    v    West Brom       
Bournemouth    v    Sunderland       
Chelsea        v    Arsenal       
Liverpool        v    Norwich       
Man City        v    West Ham       
Newcastle Utd    v    Watford       
Southampton    v    Man United       
Stoke City    v    Leicester       
Swansea        v    Everton       
Tottenham    v    Crystal Palace   
   
Septemba 26,  2015

Leicester        v    Arsenal       
Liverpool        v    Aston Villa       
Man United    v    Sunderland       
Newcastle Utd    v    Chelsea       
Southampton    v    Swansea       
Stoke City    v    Bournemouth       
Tottenham    v    Man City       
Watford        v    Crystal Palace       
West Brom    v    Everton       
West Ham    v    Norwich   
   
Oktoba 3, 2015

Arsenal        v    Man United       
Aston Villa    v    Stoke City       
Bournemouth    v    Watford       
Chelsea        v    Southampton       
Crystal Palace    v    West Brom       
Everton        v    Liverpool       
Man City        v    Newcastle Utd       
Norwich        v    Leicester       
Sunderland    v    West Ham       
Swansea         v    Tottenham       

Oktoba 17, 2015

Chelsea        v    Aston Villa       
Crystal Palace    v    West Ham       
Everton        v    Man United       
Man City        v    Bournemouth       
Newcastle Utd    v    Norwich       
Southampton    v    Leicester       
Swansea        v    Stoke City       
Tottenham    v    Liverpool       
Watford        v    Arsenal       
West Brom    v    Sunderland
       
Oktoba 24, 2015

Arsenal        v    Everton       
Aston Villa    v    Swansea       
Bournemouth    v    Tottenham       
Leicester        v    Crystal Palace       
Liverpool        v    Southampton       
Man United    v    Man City       
Norwich        v    West Brom       
Stoke City    v    Watford       
Sunderland    v    Newcastle Utd       
West Ham    v    Chelsea
       
Oktoba 31, 2015
Chelsea        v    Liverpool       
Crystal Palace    v    Man United       
Everton        v    Sunderland       
Man City        v    Norwich       
Newcastle Utd    v    Stoke City       
Southampton    v    Bournemouth       
Swansea        v    Arsenal       
Tottenham    v    Aston Villa       
Watford        v    West Ham       
West Brom    v    Leicester   
   
Novemba 7, 2015
Arsenal        v    Tottenham       
Aston Villa    v    Man City       
Bournemouth    v    Newcastle Utd       
Leicester        v    Watford       
Liverpool        v    Crystal Palace       
Man United    v    West Brom       
Norwich        v    Swansea       
Stoke City    v    Chelsea       
Sunderland    v    Southampton       
West Ham    v    Everton   

Novemba 21, 2015
Chelsea        v    Norwich       
Crystal Palace     v    Sunderland       
Everton        v    Aston Villa       
Man City        v    Liverpool       
Newcastle Utd     v    Leicester       
Southampton     v    Stoke City       
Swansea        v    Bournemouth       
Tottenham     v    West Ham       
Watford        v    Man United       
West Brom     v    Arsenal       

Novemba 27, 2015

Aston Villa     v    Watford       
Bournemouth    v    Everton       
Crystal Palace    v    Newcastle Utd       
Leicester        v    Man United       
Liverpool        v    Swansea       
Man City        v    Southampton       
Norwich        v    Arsenal       
Sunderland     v    Stoke City       
Tottenham     v    Chelsea       
West Ham     v    West Brom       

Desemba 5, 2015
Arsenal         v    Sunderland       
Chelsea        v    Bournemouth       
Everton        v    Crystal Palace       
Man United    v    West Ham       
Newcastle Utd    v    Liverpool       
Southampton    v    Aston Villa       
Stoke City    v    Man City       
Swansea        v    Leicester       
Watford        v    Norwich       
West Brom    v    Tottenham
       
Desemba 12, 2015

Aston Villa    v    Arsenal       
Bournemouth    v    Man United       
Crystal Palace    v    Southampton       
Leicester        v    Chelsea       
Liverpool        v    West Brom       
Man City        v    Swansea       
Norwich        v    Everton       
Sunderland    v    Watford       
Tottenham    v    Newcastle Utd       
West Ham    v    Stoke City