Friday, July 11, 2014

MAXIMO ANATISHA



KWELI, Kocha Marcio Maximo anatisha!, hii ni kutokana na mipango yake ya kuifundisha Yanga katika miaka yake miwili kuanzia sasa ambapo kazi hiyo itaanza rasmi leo kwenye viwanja vya bandari huku suala la vipimo likiwa ni la kwanza kufanyika.


Taarifa kutoka ndani ya kikosi hicho zimeeleza kwamba, Yanga inatarajia kuanza mazoezi hayo chini ya Maximo ambaye itakuwa ni mara yake ya kwanza kuifiundisha timu hiyo baada ya kumaliza kazi ya kuifundisha timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars.


“Kikosi cha Yanga kesho kinatarajia kuanza mazoezi yake chini ya Maximo katika viwanja vya Bandari Tandika jijini Dar es Salaam ambapo atakutana na wachezaji wote ambao hawana majukumu ya timu za taifa.


“Miongoni mwa mambo ambayo yatachukua nafasi kubwa ni kupimwa kwa wachezaji wote ili kujua hali zao za afya, pumzi zao ili kujua wapi pa kuanzia kwa lengo  la kushughulikia maeneo yenye matatizo kwa wachezaji mmoja mmoja.


“Nadhani itakuwa ni siku nzuri kwetu kama timu jambo ambalo tunaamini litakuwa ni nguzo kwetu kwani kama unavyomjua Maximo ni mtu wa watu lakini ni kocha mwenye misimamo ya kutaka kazi yake ifanyike kwa ufanisi mkubwa,” alisema mmoja wa maafisa ndani ya dawati la ufundi la Yanga.


Alhamisi wiki hii wakati anazungumza na Wandishi wa Habari, Maximo aliweka vibaombele vyake ambavyo anaamini vinaweza kuivusha Yanga hapo ilipo na kwenda mbele zaidi huku suala la kukuza na kuendeleza vipaji, nidhamu  ndani na nje ya uwanja  ni miongoni mwa mambo aliyoyatilia mkazo.


“Mipango ni mingi lakini kuna mambo ya kuyashughulikia kwa wakati huu, mopja wapo ni suala la kuendeleza vipaji vipya ambavyo naamini vinaweza kusaidia katika timu ya Yanga na Tanzania kwa ujumla, hivyo msaidizi wangu Leonadro Neiva atakuwa na kazi ya kushughulikia soka la vijana,” alisema Maximo raia ambaye kabla ya kutua Yanga alikuwa akiifundisha timu ya Associacao Atletica Francana ya jijini Sao Paulo nchini Brazil.


Dawati la unfindi la Yanga hivi sasa litakuwa na makocha watano ambao ni yeye Maximo mwenyewe kama Kocha mkuu, pamoja na wasaidizi wake watatu ambao ni Leonadro Neiva kocha msaidizi, Juma Pondamali Kocha wa makipa pamoja na Meneja Hafidh Saleh huku Kocha msaidizi mzawa akitarajiwa kujulikana baadaye.


Muungo kama huu ndiyo unaotumika kwenye nchi za Ulaya ambazo zimepiga hatua katika maendeleo ya mpira tofauti na Tanzania ambapo mfumo huu unaoneakana kuwa ni mpya.

Miongoni mwa mipango ambayo imeanza kushughulikiwa ni suala la usajili baada ya Maximo kumsajili kiungo raia wa Brazil Andrey Coutinho, ambaye anakuwa mchezaji wa tatu kutoka nje ya Afrika kusajiliwa na Yanga tangu kuanzishwa kwake mwaka 1934.


Yanga inalazimika kufanya usajili huo kutokana na kuwepo kwa pango la wachezaji wawili tegemeo ambao ni kiungo Frank Domayo na shambuliji raia wa Burundi, Didier Kavumbagu ambao wote waiwli wametimkia Azam FC hivyo ujio wa Countinho ni moja ya dawa ya kuhakikisha kikosi chake kinakuwa bora.


Hii si mara ya kwanza kwa Yanga kusajili wachezaji kutoka nje ya Afrika ambapo kwakwani kwa mara ya kwanza, ilimsajili kipa  kutoka nchini Serbia Obren Cirkovic katik usajili wa mwaka 2008.


Kutokana na ubora wake, kipa huyo aliweza kuwa kipa namba moja ndani ya kikosi cha Yanga ingawa alikuwa akibadilisha na kipa Juma Kaseja katika baadhi ya mechi huku timu hiyo ikiwa chini ya Kocha raia wa Serbia Dusan Kodic.

Kadhalika katika msimu wa mwaka 2010,  Yanga iliandika historia nyingine baada ya kumsajili kipa kinda kutoka Serbia, Ivan Knezevic ambaye alidumu kwa misimu miwili kisha kutimkia katika klabu ya FK Novi Sad ya Serbia.



No comments:

Post a Comment