Tuesday, July 1, 2014

Yanga wakana dau la Ngassa


Marcio Maximo, Kocha wa Yanga

KLABU ya Yanga, imesema kuwa haijapata ongezeko la dau la kumnunua nyota wao, Mrisho Ngassa kutoka klabu ya Free State Stars ya Afrika Kusini.

Baada ya kufuzu katika majaribio hayo, imeelezwa kuwa klabu hiyo ya Afrika Kusini ilituma ofa kwenda Yanga ambayo ni Doa za kimarekani 80,000 zaidi ya milioni 134 fedha za Kitanzania ingawa ofa hiyo ilikataliwa kwani Yanga walikuwa kihitaji Dola 150,000, zaidi ya milioni 250.

Hata hivyo dira ya ulimwengu ilimtafuta Mwenyekiti wa mashindano wa Yanga ambaye pia mara kadhaa amekuwa akishughulikia usajili, Seif Ahamed ‘Magari’ alikana kuwa Yanga ilitaka dao hilo la Dola 150,000 ingawa hakutaja kiasi gani kilichopendekezwa. 
“Mimi ninafahamu kwamba ofa kutoka Afrika Kusini ilifika mezani kwetu lakini fedha zilinazoelezwa si za kweli ila kuna makubaliano ambayo yapo baina ya klabu zote mbili yaani Yanga pamoja na  Free State Stars, ingawa kwa maelezo zaidi zungumza na Katibu Beno Njovu au Msemaji Baraka Kizuguto,” alisema Magari ambaye amerejea hivi karibuni akitokea Brazil kuangalia michuano ya Kombe la dunia. 

DIMBA lilimtafuta, Kizuguto alisema alisema suala la kuongezwa dau hajaipata yeye kama msemaji na kwamba sujala la biashara ya kumuuza Ngassa katika klabu ya Free State linafanywa na pande mbili ingawa hakuweza kufafanua zaidi.

 “Ninachokifahamu ni kwamba Yanga ilimruhusu Ngassa kwenda Afrika Kusini kufanya majaribio pamoja na kambi ya timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars iliyopo nchini Bostwana. 

Katika hatua nyingine, Kocha wa Free State ya Afika Kusini, Mbelgiji, Tom Saintfiet amemtabiria mambo makubwa Mrisho Ngassa  ikiwemo kucheza soka barani Ulaya kama akifanikiwa kujiunga na klabu hiyo.

“Kwanza Free State wenyewe hatukaa naye muda mrefu ila soko la kwenda Ulaya hapa ni kubwa ikilinganisha na maeneo mengine ya Afrika kwa hiyo kama akifanikiwa kucheza katika kikosi chetu ni wazi kuwa milango ya ulaya ipo wazi kulingana na falsafa za klabu hii,” alisema Saintfiet, Kocha wa zamani wa Yanga na timu za taifa za Ethiopia na Malawi.

Ngassa yupo Afrika Kusini kwa ajili ya kufanya majaribio ya kucheza soka ya kulipwa katika klabu hiyo ya Free State Stars inayonolewa na kocha wa zamani wa Yanga, Mbelgiji Tom Saintfiet na tayari imeelezwa kuwa amefuzu.

SALMA JUMA NA SAADA AKIDA  wa DIMBA

No comments:

Post a Comment