Tuesday, July 1, 2014

Wabunge wa CPA Tanzania watembelea Hifadhi za Taifa

Mwenyekiti wa Chama cha Wabunge la Jumuiya ya Madola (CPA) tawi la Tanzania, Mh. Mussa Zungu akizungumza na Katibu wa Bunge,Dk.Thomas Kashililah(kulia)wakiwa kwenye ziara ya tathmini ya Maandalizi ya Mkutano wa 45 wa CPA utakaofanyika jijini Arusha mwezi huu,jana walipotembelea Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara mkoa wa Arusha,kushoto ni Meneja Uhusiano wa Tanapa, Pascal Shelutete na katikati Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi hiyo, Domician Njau.
 
2 
 Afisa Utalii wa Hifadhi ya Ziwa Manyara, Jully Lyimo(wa pili kushoto)akiwaongoza Wabunge na Maafisa wa Bunge waliotembelea Hifadhi hiyo jana.

 
3
 Mwenyekiti wa Chama cha Wabunge la Jumuiya ya Madola (CPA) tawi la Tanzania, Mheshimiwa Mussa Zungu akiwa na Wajumbe wa Bunge hilo na Maafisa wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kwenye Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara hivi karibuni.

  4 
 Mwenyekiti wa Chama cha Wabunge la Jumuiya ya Madola(CPA)tawi la Tanzania,Mheshimiwa Mussa Zungu(kulia)akizungumza jambo wakati Wajumbe wa Bunge hilo wakiwa kwenye ziara ya tathmini ya Maandalizi ya Mkutano wa 45 wa CPA,jana walitembelea Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara mkoa wa Arusha,kushoto ni Wajumbe wa CPA, Beatrice Shelukindo na Mhonga Ruhwanya.

 
Mwikolojia wa Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara,Yustina Kiwango akizungumzia hali ya Hifadhi hiyo kwa Wajumbe Chama cha Wabunge wa Jumuiya ya Madola tawi la Tanzania(CPA)waliotembelea ikiwa ni maandalizi ya Mkutano mkubwa utakaofanyika mwezi huu jijini Arusha.
 
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Tarangire, Stephano Qolli akitoa taarifa fupi ya Hifadhi hiyo kwa Wajumbe wa Bunge la Jumuiya ya Madola(CPA)tawi la Tanzania wakiwa kwenye ziara ya tathmini ya Maandalizi ya Mkutano wa 45 wa CPA walipotembelea Hifadhi hiyo.

  7
Mwenyekiti wa Chama cha Wabunge la Jumuiya ya Madola(CPA)tawi la Tanzania,Mheshimiwa Mussa Zungu(katikati)akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wake,Wafanyakazi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Wafanyakazi wa Hifadhi ya Taifa ya Tarangire jana.

No comments:

Post a Comment