Saturday, August 16, 2014

samaki wa Arapaima huyu hapa


Samaki aliye na urefu wa mita tatu aliyekuwa maarufu katika mto Amazon amevuliwa hadi ameangamia.
Watafiti wamedhihirisha kuwa samaki huyo mkubwa hapatikani tena katika maeneo aliyokuwa maarufu.
Imebainika sasa kuwa samaki wa Arapaima alipatikana katika maeneo 8 kati ya 41 zilizofanyiwa utafiti, na idadi ya samaki huyo ilikuwa ndogo sana kulikoilivyokuwa inatarajiwa.
Wavuvi walipewa mafunzo jinsi ya kuhesabu samaki hao ili kufanikisha utafiti huo mkubwa.
Watafiti walikata kauli kuwa athari za uvuvi kwa samaki wa kitropiki zilikuwa mbaya zaidi ya ilivyoaminika hapo awali.
Matokeo ya utafitihuo yaliripotiwa kwa shirika la uhifadhi wa mazingira yanayozalisha viumbe vya majini ''Aquatic Conservation: Freshwater and Marine Ecosystems''.
Arapaima huweza kuwa na uzani wa kilo 181 na ni mojawapo ya samaki wakubwa zaidi wanoishi katika maji yasiyo na chumvi.
Samaki hao hupumua hewa sawa na binadamu, hivyo basi huibuka kutoka majini kupumua kila baada ya dakika kati ya 10-15 hivyo basi huwa ni rahisi kuwakamata.
Ukubwa wa Arapaima huvutia wavuvi kuwawinda na aghalabu huwanasa kwa kutumia chusa au nyavu za uvuvi.
Karne moja iliyopita, idadi ya Arapaima ilikuwa kubwa katika mto wa Amazon, lakini watafiti wanasema kuvua kupita kiasi kumesababisha idadi hiyo kupungua kwa kiwango kikubwa sana.
Hapo awali, utafiti nadharia ulitabiri kuwa uvuvi hauwezi kuangamiza aina fulani ya samaki majini kwani wavuvi huenda kuvua maeneo tofauti idadi ya samaki inapopungua katika eneo moja.
Wanasayansi, wakiongozwa na Leandro Castello, kutoka Virginia Marekani, walitaka kufahamu afya ya samaki wa Arapaima walioko eneo la chini la Amazon.
Aidha walitaka kugundua iwapo shughuli za uvuvi ziliunga mkono au kupinga utabiri wa nadharia tofauti.
Kuna nadharia zinazopendekeza kuwa samaki wakubwa, walio ghali, na ambao ni rahisi kukamatwa huweza kuvuliwa na kuisha majini, huku nadharia zingine zikipinga msimamo huo.
Watafiti hao walihoji wavuvi 182, walioaminika kuwa magwiji na wenzao, katika jamiii 81, zinazoishi katika eneo la kilomita 1,040, la Amazon.
Shughuli hiyo ilijumuishwa hesabu ya Kulifanywa ya samaki katika jamii 41 kati ya jamii zilizohojiwa.
Wavuvi nane walifunzwa kuhesabu idadi ya Arapaima pindi tu walipotokea majini.
Matokeo ya hesabu hiyo ni kuwa idadi ya Arapaima ilikuwa imepunguka katika asilimia 57% ya eneo la utafiti, Arapaima hawakuwepo katika asilimia 19% ya eneo hilo, na walivuliwa kupita kiasi katika asilimia 17% ya eneo hla utafiti, huku asilimia 5% tu wakifanya uvuvi unaokubalika.
Kwa 2% ya jamii zilizofanyiwa utafiti, samaki hao hawakuvuliwa.

Chanzo cha bbc.swahili 

Man United kuzoa pointi 18 za fastafasta





NA EZEKIEL TENDWA
LIGI Kuu ya England inatarajiwa kuanza rasmi mwishoni mwa wiki ijayo ambapo nyasi za viwanja mbalimbali zitawaka moto kila timu ikihitaji kujikusanyia pointi za mapema mapema kabla ligi yenye haijachanganya.

Timu zote zimekuwa zikifanya maandalizi ya nguvu kwa ajili ya kuhakikisha wanafanya vizuri wengine wakitaka kuchukua ubingwa na wengine kuepuka mkasi wa kushuka daraja kwani katika soka kila mmoja ana malengo yake.

Katika ratiba iliyotolewa na chama cha soka nchini humo FA, inaonekana kuwabeba Manchester United katika michezo yao sita ambapo kama wataingia na moto waliouonyesha nchini Marekani kwenye mechi za kujiandaa na ligi hiyo, ambapo kama mwendo utakuwa huo huo watajikuta wakikusanya pointi 18 za mapema bila kikwazo chochote.

Wakiwa nchini Marekani mabingwa hao wa zamani wa  England waliwatoa nishai vigogo kama Los Angeles Galaxya Marekani, AS Roma na Inta Milan zote zinazoshiriki Ligi Kuu ya Italia, Real Madrid ya Hispania pamoja na Liverpool ya England.

Kikosi hicho ambacho kipo chini ya kocha wao mpya Louis Van Gaal kitaanza mchezo wao wa kwanza Jumamosi ya wiki ijayo dhidi ya Swansea, licha ya wapinzani wao kuwa katika kiwango kizuri lakini uwezo wa kutoa upinzani kwa Mashetani Wekundu  hao ni mdogo ingawa kwenye soka lolote linaweza kutokea.

Mchezo wa pili kwa Van Gaal na kikosi chake itakuwa dhidi ya Sunderland uwanja wa ugenini ambapo katika msimu uliopita Sunderland licha ya kuwatoa kijasho Man United lakini historia inaweza ikaendelea kuwabeba Man United.

Agosti 30 Man United, watakuwa tena ugenini kukipiga na Burnley FC ukiwa mchezo wa tatu ambapo kutokana na ari ya ushindi waliyonayo watataka kuondoka na pointi ili tu kujiwekea mazingira mazuri ya kuhakikisha wanatafuta nafasi ya kushiriki michuano ya UEFA.

Wakati Arsenal wakiwa na kibarua cha kuwakabili mabingwa watetezi wa michuano hiyo Manchester City katika uwanja wao wa Emirates Septemba 13, kwa upande wao Man United wataendelea kujitafutia pointi nyingine katika uwanja wao wa Old Trafford dhidi ya QPR Septemba 14.

Van Gaal atakuwa tena na kibarua cha kutafuta pointi kwa timu ndogo ya Leicester ugenini Septemba 20 kabla ya kumalizia kubarua cha kucheza na dhidi ya West Ham Septemba 27 kwenye uwanja huo huo wa jijini Manchester.

Hiyo ndiyo michezo sita ambayo kwa vyovyote Manchester United watatakiwa kutafuta pointi 18 kabla ya kuanza kukwaana na vigogo ambapo baada ya michezo hiyo watavaana na wabishi Everton kabla ya kupata mteremko mwingine dhidi ya West Bromwich Albion na baadaye kuja kucheza na Chelsea 0ktoba 26.

Arsenal wao wataanza kwa mteremko kidogo mchezo wa kwanza watakapocheza na Crystal Palace na baadae kukutana na wabishi Everton ugenini huku Manchester City wao wakianza na wagumu Newcastle kabla ya kuwavaa Liverpool.

Timu hizi kubwa za Manchester United, Manchester City, Liverpool, Arsenal, pamoja na Chelsea ndizo zinazotafuta nafasi nne za kwanza ili kupata tiketi ya kushiriki UEFA ambapo msimu huu Manchester United wamepigwa kumbo baada ya kumaliza wakiwa nafasi ya saba msimu uliopita.

Kwa maana hiyo ni kwamba msimu ujao Ligi Kuu England itakuwa moto wa kuotea mbali kwani timu hizi vigogo moja lazima iwapishe wenzake kwani sheria inaruhusu timu nne tu kutinga kwenye michuano hiyo ya UEFA inayoheshimika duniani kote.

Wednesday, August 13, 2014

Mainda: Wasanii wengi maisha yao ni ya filamu



NA JENNIFER MANONI
RUTH Suka ni mwigizaji wa siku nyingi kutoka katika Kundi la Kaole Sanaa lililokuwa linatamba miaka ya nyuma na maigizo yake yaliyokuwa yanaonyeshwa kupitia televisheni ya ITV.
Mwanadada huyo ni miongoni mwa waigizaji wengi wanaofanya vizuri kwa sasa kwenye tasnia ya filamu Tanzania na Afrika Mashariki na Kati kwa ujumla.
Miongoni mwa waingizaji hao waliokuwa wanaunda kundi la Kaole wakati huo ni pamoja na Vicent Kigosi ‘Ray’, Hissan Muya ‘Tino’, Muhsin Awadh ‘Dr Cheni’ Elizabeth Michael ‘Lulu’, Marehemu Steven Kanumba, Blandina Chagula ‘Johari’ na wengine wengi.
Kupitia safu hii Dimba lilipata fursa ya kuzungumza na mwanadada huyo kwa ajili ya kujua mambo muhimu matano kutoka kwake ambayo yamekuwa ni sehemu ya mafanikio yake tangu alipoanza maisha yake ya filamu.
UPENDO
“Wasanii kwa sasa hatupendani hata kidogo hadi pale unapotokea msiba au sherehe ndiyo utawaona wakikaa pamoja na kujifanya wanampenda mtu ila wakati alipokuwa hai au alipokuwa na matatizo wanaishia kumsema pembeni tu, ila hii imenifanya kufanya kazi kwa bidii na kujitegemea badala ya kutegemea watu wengine.
CHANGAMOTO
“Changamoto kubwa katika kazi yangu ni wasanii wengi kutojali muda wa kufika kwenye eneo la kurekodia ‘location’ na mara kadhaa hii iankuwa nio tofauti na vile mnavyokubaliana. Mambo haya wakati mwngine najiuliza ni kwa nini mtu anafanya hivi au kuna nia ya kuniharibia kazi ila ndiyo hali ya watu ninaofanya nao kazi.
MAISHA YA WASANII
“Maisha ya wasanii ni mabaya ila wanalazimisha kuishi hivyo kwa kulazimisha kutokana na majina yao na ndiyo sababu wanajitahidi kubadilisha nguo na magari ambayo yanakuwa kitendawili kama ni ya kwao au wanayaazima. Kifupi maisha yao ni ya filamu au maigizo si maisha halisi.
MALENGO
“Kwa sasa nimesimama kwa muda naangalia kwanza soko la filamu linavyokwenda ili kama nitakuja kutoa filamu iwe na maana na siyo kulazimisha kutoa kazi nyingi zisizoeleweka. Kutokana na hilo naweza ukajikuta unauza jina badala ya kutafuta pesa kwa sanaa kwa sasa ni zaidi ya kazi na sio starehe peke yake na kuwafurahisha tu watu.
STAREHE
“Wasanii tumeweka starehe mbele kuliko kazi hiyo yote ni kutokana na kuridhika mapema kwa vijisenti anavyochukua au anavyopata kutokana na kazi husika, hili ni tatizo ambalo lazima sasa wasanii wenyewe wabadili fikra zao,” anasema nyota huyo.


Hapa ndipo Cecafa ilipochemka



JUMAPILI iliyopita katika gazeti la DIMBA nilizumzia suala lilaloendelea kutokota Afrika Mashariki na Kati hasa baada ya Yanga kuenguliwa kwenye michuano ya Kombe la Kagame mwaka huu.
Wapo ambao walinipinga na wengine waliniunga mkono, binafasi niwapongeze wote na kuwashukuru kwani wameonyesha ukomavu wa hali ya juu wa kupembua mambo.
Lakini kutokana na unyeti wenyewe na uzalendo wangu kwa Tanzania, nimeamua kuamalizia baadhi ya mambo niliyoona yanastahili kufafanuliwa ili jambo hili liweze kueleka sawa.
Pia kuepusha baadhi ya watu kutowafanya Watanzania kisima cha fedha au ghala la fedha, kama wanavyotaka kufanya baadhi ya viongozi wa Baraza la vyama vya soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa).
Mfano kwenye Kombe la Kagame msimu huu Yanga iliondolewa Cecafa kwa madai ya kupeleka wachezaji wa timu B badala ya A. Hiyo ndiyo ilikuwa sababu ya msingi ambayo Cecafa kupitia Katibu Mkuu wake Nicholas Musonye iliueleza umma wa wapenda soka Afrika Mashariki na Kati kwamba suala la timu B ndiyo dhambi kubwa iliyoigharimu Yanga.
Awali niunga mkono maamuzi ya Cecafa lakini baada ya kufanya utafiti wa kina niliweza kugundua makosa na udhaifu mkubwa katika jambo hili ingawa suala la kipato ndilo lililochukua nafasi kubwa badala ya kweli wa mambo kwa liugha rahisi ni kwamba Cecafa haikusema kweli.
Kama Yanga ingekwenda singekuwa timu pekee iliyopeleka wachezaji vijana ila timu zilichukua hatua hiyo ni nyingi lakini kutokana na umaarufu wa timu za Tanzania hasa Simba na Yanga ndiyo nongwa ilianzia hapo.
Kwa mfano katika michuano ya mwaka huu kuna klabu ya Ethiopia iitwayo Adama City Oromiya FC ‘Nazareth’ ambayo ilipeleka vijana, hivyo kwa uelewa wa kawaida tu ni kwamba kuna tatizo kwenye suala la kuchukuliwa kwa maamuzi haya kwani mbona Adama City haikuondolewa?.
Najiuliza je? hawa Adama City wachezaji wao wa timu B ni tofauti gani na wale wa kikosi B cha Yanga. Ndiyo maana nasema katika jambo hili Cecafa ilikosea au ilichemka kama wasemavyo vijana wa kizazi cha sasa.
Ili kuonekana kuwa Cecafa ilipotea njia ni kwamba kanuni zake za wachezaji wanaotakiwa kucheza kwenye michuano ya Kagame, wanatakiwa wenye leseni ya shirikisho la nchi kusika yaani kama ni timu kutoka Tanzania lazima mchezaji awe na leseni kutoka shirikisho la soka la nchi husika.
Nilifikiri kwa sababu Cecafa haina michuano yoyote ya umri ingeona fahari kuwatumia vijana zaidi ili kuwasaidia ikiwemo kutoka katika nchi zao na kwenda kwenye nchi nyingine ndani na nje ya ukanda huu badala ya kuendelea kuwa na mawazo ya kizamani ya kuwategemea wachezaji wale wale.
Kwa hiyo Yanga haikukosea kwa lolote na ilikuwa na haki ya kuamua imtumia nani na imuache nani kwenye michuano ya mwaka huu kwani hata hakuna kanuni inayoibana juu ya kuwatumia wachezaji wa aina gani, kwa lugha rahisi naweza kusema baraza hili linapiga siasa badala ya kufanya maendeleo.
Sasa Cecafa ilitakiwa iwaeleze wadau wa soka kwamba wachezaji wa Yanga waliokuwa wapelekwe kwenye michuano hiyo hawakuwa na leseni ya TFF jambo ambalo si kweli ila walikuwa wameangalia zaidi fedha zinatakazopatikana kutokana na viingilio kwani wangekuwepo akina Mbuyu Twite na wenzake mashabiki wangeongezeka mara dufu.
Ndiyo maana nasisitiza kwamba jambo hili limechukuliwa kwa hasira na kukurupuka tofauti na ukweli ulivyo.
Kwa mazingira haya naendelea kusimamia msimamo wangu kwamba Cecafa ilikosea na ilifanya maamuuzi ya kukurupuka kwani hata leo ukiwauliza kwamba wanaijua ‘first eleven’ ya Azam FC iliyochukua nafasi ya Yanga, au Adama ya Ethiopia ni wazi kwamba hawazijui ila kwa sababu ya umaarufu ya wachezaji wa Yanga ndiyo waliouangalia.

Mwenendo huu wa Cecafa naamini unastahili kubadilika hasa kutokana na umri wake kwenye masuala ya kuendeleza soka Afrika kwa sababu hadi leo baraza hili limeshafikisha umri wa miaka 88.
Kwa umri huu nilitegemea soka la Afrika Mashariki na Kati lingevuka kutoka hapa na kwenda mbele ila imekuwa kinyume kwani maendeleo yake ni madogo na hafifu ikilinganishwa na kanda nyingine.
Kwenye ulimwengu wa sasa suala la uweledi na ukweli ndiyo unaweza kuleta tija na maendeleo lakini kutokana na aina ya viongozi tuliokuwa nao hatuwezi kufika popote kwani wengi wao si wakweli katika utendaji wao.
Kama kweli ukanda huu na Cecafa tunahitaji kufanikiwa lazima badaliko ya kiutendaji yafanyike vinginevyo tunaishia katika soka la wahapahapa na kuziacha nchi nyingine kuendelea mbele.
Pia Cecafa inastahili sasa kuangalia namna ya kupata wadhamini wa mashindano yao badala ya kutegemea viingilio kutoka kwa timu za Tanzania ambazo hasa Simba na Yanga ambazo zimeonekana kuwa na mvuto kwa mashabiki tofauti na timu nyingine za ukanda huu.
Hili likifanyika tunaweza kufanikiwa na kupiga hatua kwani kutakuwa na mfumo bora wa kurithisha vipaji kutoka kikazi kimoja khadi kingine badala ya kuendelea kuwategemea wachezaji wale wale wa miaka yote.
Kama Cecafa itakuwa ikiwategemea Juma Kaseja, Emmanuel Okwi, Haruna Niyonzima na wengineo ili kuendesha michuano yao itakuwa ni hatua ya juu ya kushindwa badala ya kushinda. 

Mwandishi wa makala haya ni Ahadi Kakore-0784890387

Simba itatisha tu-Kiongera



NA SAADA AKIDA
KOMBINESHENI ya Mastraika wawili wa Kimataifa wa Simba, Paul Raphael Muigai Kiongera na Amis Tambwe imelikuna benchi la ufundi la timu hiyo lililokuwa likiongozwa na Zdravko Logarusic kabla ya kufukuzwa Jumapili iliyopita.
Awali klabu hiyo ilikuwa inamtegemea Tambwe pekee katika safu ya ushambuliaji ambapo alimaliza msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara akiibuka mfungaji bora kwa kufunga mabao 19.
Breaking News lilishawishika kufanya mahojiano na mshambuliaji huyo raia wa Kenya ambapo katika mazingumzo hayo aliweza kueleza mambo mambalimbali ambayo anaamini yamemfanya kuwemo kwenye kikosi cha Simba msimu huu.
USAJILI WAKE SIMBA:
Kiongera aliyekuwa anakipinga KCB inayoshiriki Ligi Kuu Nchini Kenya anasema alitoa kwa maa ya kwanza ndani ya Simba ilikuwa kwa ajili ya mazungumzo na kurejea Kenya kwa ajili ya kuchukuwa kibali katika klabu yake ya zamani ya KCB FC.
 “Nipo Simba kwa muda wa miaka miwili baada ya kumalizika taratibu zote hivyo kwa sasa nitakuwa nikifabya kazi Tanzania,” anasema nyota huyo.
NINI ATAKACHOKIFANYA:
Anasema anachohakikisha ni kutoa ushirikiano mzuri na wachezaji wenzake kufikia malengo ya na matakwa ya timu ambayo ni kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
“Nimekuja kufanya kazi Simba, moja ya vitu ambavyo nahitajika ni kuhakikisha tunafanya vizuri kwa kupata ushindi, hasa katika ligi ambapo ndiyo kielelezo cha mafanikio kuelekea kwenye mashindanio makubwa ya kimataifa,” anasema.
UPACHA WAKE NA TAMBWE:
 “Unajua nimejiunga siku moja kabla ya mchezo huu (dhidi ya Zesco), kwa hiyo ilikuwa ngumu kuelewana haraka na Tambwe lakini niliweza kumsoma na kumjua haraka jinsi gani natakiwa kumtumia vizuri, naamini kama tukuenda kwa mwendo huu tunaweza kufanya makubwa siku zijazo,” anasema.
Kiongera anasema Tambwe ni mchezaji mzuri jamboa ambalo linampa matumaini ya kufanya vizuri kwa siku zijazo ndani ya kikosi hicho ambacho chenye maskani yake mtaa wa Msimbazi jijini Dar es Salaam.