Tuesday, October 28, 2014

Dogo Aslay: Siku ya Msanii imetupa heshima




NA MWANDISHI WETU

KIONGOZI wa kundi chipukizi la muziki wa dansi nchini, Yamoto Band, Dogo Aslay, amefunguka kuwa ushiriki wao kwenye tamasha la 'Siku ya Msanii' umeijengea heshima bendi hiyo.
Aslay ameliambia DIMBA Jumatano kwamba, tamasha hilo lilikuwa na sura ya kitaifa hivyo kupata kwao nafasi ya kutumbuiza kutawasaidia kuongeza mashabiki na kuheshimika kama ilivyo kwa bendi kongwe za muziki wa dansi nchini.
"Kwetu tunawapigia saluti waandaji wa siku ya msanii kutuchaguza kuwa watumbuizaji kwani Tanzania kuna bendi nyingi lakini tukawa pekee kupata nafasi hiyo.
Katika tamasha hilo wasanii Edward Said Tingatinga alitunukiwa tuzo ya Msanii aliyejitolea maisha yake yote katika maendeleo ya sanaa (Lifetime achievement award) na Josephat Kanuti kutoka Morogoro, ambaye alitunukiwa tuzo ya msanii aliyetoa mchango mkubwa katika jamii kupitia sanaa (Humanitarian award).
Siku ya Msanii Tanzania, iliandaliwa na kampuni ya Haak Neel Production na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) na kudhaminiwa na Kampuni ya New Habari (2006) Ltd, wachapishaji wa magazeti ya Bingwa, Dimba, Rai, Mtanzania na The African, Azam Media, Hugo Domingo, EFM, Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Channel Ten na Magic FM.

No comments:

Post a Comment