Wednesday, April 22, 2015

Simba yamtengea Msuva Ml. 170

NA SAADA SALIM
KAMATI ya Usajili ya Klabu ya Simba imetenga Sh milioni 170 kwa ajili ya kumnasa winga machachari wa Yanga, Simon Msuva, ili aisaidie timu hiyo katika msimu ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu ujao.

Taarifa zisizo na shaka zilizolifikia DIMBA Jumatano kutoka kwa kigogo mmoja wa Kamati hiyo zinaeleza kuwa tayari wameshatenga donge hilo kwa ajili ya kumnasa Msuva, ambaye amekuwa na msimu mzuri ndani ya Yanga kutokana na kuwa mwiba mkali wa kucheka na nyavu.
"Suala la Msuva kuja Simba halina ubishi wowote, kwani Kamati inaendelea na harakati za kumnasa winga huyo kwa ajili ya msimu ujao," alisema kigogo huyo na kuongeza: "Dau hilo tulilomtengea tuna uhakika kabisa hawezi kulikataa".
Kwa nyakati tofauti Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Kepteni Zacharia Hanspope, amekiri uwepo wa mpango wa kuipa pigo Yanga kwa kumchukua Msuva kwa madai kuwa kiwango chake ni kizuri na pia hata yeye mwenyewe anaipenda Simba, hivyo hawana budi kumrejesha nyumbani.

No comments:

Post a Comment