Wednesday, March 30, 2016

Azam macho yote kwa Prisons kesho

NA SALMA MPELI
UONGOZI wa timu ya Azam FC umesema kuwa kwa sasa macho yao yote yapo kwa Tanzania Prisons ambao wanatarajia kukutana nao kesho ikiwa ni mechi ya Kombe la Shirikisho (FA) mchezo utakaopigwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.

Akizungumza na DIMBA, Ofisa Habari wa Azam, Jafari Idd, alisema hiyo ndiyo mechi iliyoko mbele yao kwa sasa kabla ya ile ya ligi dhidi ya Toto African ya Mwanza, Aprili 3 kabla ya kukutana na Esperance ya Tunisia kwenye Kombe la Shirikisho.
“Tunajiandaa kuhakikisha tunaibuka na ushindi ili kuingia hatua ya nusu fainali, tunashukuru kikosi chetu kimekamilika baada ya wachezaji wa timu ya Taifa kurejea na kujiunga kambini pamoja na wenzao,” alisema Jaffer.
Katika msimamo wa Ligi Kuu Azam wapo nafasi ya tatu wakiwa na pointi 50 sawa na Yanga huku zikitofautiana idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa.

No comments:

Post a Comment