Wednesday, March 30, 2016

Manara: Al Ahly iifunge Yanga 5-0

NA EZEKIEL TENDWA
UNAKUMBUKA yale mabao 5-0 ambayo Simba waliwafunga Yanga msimu wa 2012? Sasa ni hivi, msemaji wa Wanamsimbazi hao, Haji Manara, amesema anataka Al Ahly iibuke na ushindi kama huo dhidi ya Wanajangwani hao Jumamosi ya Aprili 9.
Unajua kwanini Manara ameamua kutamka maneno hayo? Jibu ni jepesi tu kwamba kama Yanga wataibuka na ushindi dhidi ya Al Ahly katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jiji halitakalika.
“Nataka Yanga ifungwe mabao 5-0 kama tuliowafunga sisi mwaka 2012 kwani hawa Yanga wakishinda mji hautakalika. Nadhani ikiwa hivi mambo yatakuwa sawa sawa na mji utakalika na kahawa itanyweka,” alisema Manara mtoto wa nyota wa zamani wa Yanga, Sunday Mnara ‘Computer’.
Yanga na Al Ahly zinatarajiwa kukutana Aprili 9 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, mchezo wa mabingwa barani Afrika.

No comments:

Post a Comment