Wednesday, March 30, 2016

Habari njema kwa Wajasiriamali wadogo na wakati

Kutokana na mahitaji ya matangazo kuwa makubwa na baadhi ya watu hasa wenye kipato cha chini kushindwa kuyamudu, dirayaulimwengu imeamua kupunguza bei zake za matangazo madogo madogo hadi kufikia shilingi 35, 000/= kwa tangazo moja kwa wiki (siku saba).
Hivyo wajasiriamali na wale wenye biashara ndogo kama maduka ya nguo, maduka ya vyakula, wakulima, wauza vinywaji, wamiliki wa bar na night club, wamiliki wa shule au vyuo, wakati wao kuwafikia maelfu ya watu kupitia mtandao huu. Kwa wale wenye mahitaji wawasiliane na idara ya matangazo kwa simu namba 0784 890 387. 

RAIS MAGUFULI ATOA HATI YA KIWANJA KWA MSD



Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi (kushoto), akimkabidhi hati ya kiwanja chenye ukubwa wa ekari tano Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu kilichotolewa na Rais Dk. John Magufuli kwa MSD kupitia Wizara hiyo Dar es Salaam leo mchana.Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu (kulia), akisalimiana Naibu Katibu Mkuu wa  Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Moses Kusiluka wakati wa hafla hiyo ya kukadhiana hati hiyo ya kiwanja. Katikati ni Waziri wa Wizara hiyo, William Lukuvi.
 Salamu zikiendelea. Hapa Mkurugenzi Mkuu wa MSD, akisalimiana na Mkurugenzi wa Mipango Miji, Profesa John Modestus.
 Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu (mbele kulia), akizungumza kwenye hafla hiyo.
 Waziri Lukuvi na Mkurugenzi wa MSD, wakiangalia hati hiyo.
Viongozi wa wizara hiyo wakiwa kwenye mkutano hafla hiyo. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Idara ya Usanifu Majengo, Amina Ramadhani, Ofisa Ardhi Mkuu, Mwamasage na Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani, Justo Lyamuya.

Na Dotto Mwaibale
RAIS Dk. John Magufuli kupitia Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi  ametoa kiwanja chenye ukubwa wa ekari 5 kwa Bohari ya Dawa (MSD) kilichopo Luguluni nje kidogo ya jiji la  Dar es Salaam, kwa ajili ya ujenzi wa Bohari ya Dawa ili kuondoa upotevu wa fedha kwa maghala ya kukodi.

Ujenzi wa maghala katika kiwanja hicho utaokoa kiasi cha sh. bilioni 4 zilizokuwa zikitumika kila mwaka kwa ajili ya malipo ya maghala ya kukodi yaliyopo Mabibo Ubungo jijini pamoja na kanda mbalimbali  nchini.

Akizungumza wakati wa akikabidhi hati hiyo kwa Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu Dar es Salaam leo mchana,  Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi alisema, Rais ametoa ardhi hiyo ili kuepusha gharama zisizo na sababu kwa MSD.

Alisema agizo la rais fedha zilizokuwa zikitumika kwa ajili ya kukodi maghala hayo, zinapaswa kununua dawa ili kila Mtanzania apate huduma bora za kiafya.

“Rais aliniagiza niwape eneo, leo nimetekeleza agizo hilo kilichopo muanze ujenzi kama mlivyoomba kwa ajili ya kujenga ghala la dawa, naamini mtaanza mara moja balada ya kuendelea kukodi maghala na  badala yake fedha zote zitumike kwa ajili ya kununulia dawa na vifaa tiba,” alisema Lukuvi na kuongeza;

“Kiwanja hiki ambacho kilikuwa cha Shirika la Taifa la Nyumba (NHC) kilichokuwa na ukubwa wa ekari 200, tumewapa ekari tano kama uhitaji wenu ulivyokuwa, nimewasamehe kodi ya premium na badala yake kiasi cha Sh16.7 hamtalipa na gharama mtakayotakiwa kulipa ni sh. milioni 2 pekee ili muanze ujenzi mara moja.”

Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa  (MSD) Laurean Bwanakunu alisema tayari wameshazungumza na Bodi ya wadhamini, Wizara ya Afya na wahisani hivyo ujenzi unatarajiwa kuanza mara moja Julai Mosi.

“Tunamshukuru sana Rais kwa sababu ombi hili limefanyiwa kazi kwa haraka sisi kama MSD tulishindwa kuhimili mikiki kutokana na gharama kubwa iliyokuwa ikielekezwa katika malipo ya ghala la kukodi pale ubungo mwaka wa fedha ulioisha tulilipa kiasi cha Sh3.5 bilioni na tukitarajia mwaka huu mpya wa fedha inafikia Sh4 bilioni kwa sababu ya malipo kwa dola,” alisema Bwanakunu.

Alisema katika eneo hilo jipya lililopo Luguluni wanatarajia kujenga zaidi ya maghala matano yenye ukubwa wa sikwea mita mita 5000 yatakayogharimu kiasi cha sh. bilioni 10nkila mojawapo, “ujenzi huu utakapokamilika kanda zitakazonufaika ni pamoja na Dar es Salaam, Morogoro na Pwani na kuwa eneo hilo walilopata wanaweza kujenga kiwanda cha maji. (Imeandaliwa na Dotto Mwaibale)

Msuva ampa Tambwe kiatu cha dhahabu

NA ZAINAB IDDY
LICHA ya mshambuliaji wa Simba, Hamis Kiiza, kuongoza katika mbio za ufungaji bora, mfungaji bora wa msimu uliopita, Simon Msuva wa Yanga, amesema kwamba Mrundi, Amis Tambwe, ndiye atakayeibuka mfungaji bora msimu huu.
Msuva amelisema kwamba, licha ya Tambwe kupata upinzani mkali kutoka kwa Kiiza, lakini ana nafasi kubwa ya kupata tuzo hiyo msimu huu kutokana na uwezo wake wa kupachika mabao.
 “Najua upinzani katika mbio hizo za ufungaji bora ni mkubwa lakini kwangu mimi nampa nafasi kubwa Tambwe kwani anao uwezo mkubwa wa kutumia nafasi anazozipata,” alisema Msuva.
Tambwe ambaye msimu wa 2013/14 aliibuka mfungaji bora akiwa na mabao 17 wakati huo akiichezea Simba, kwa sasa ana mabao 17, nyuma ya Kiiza mwenye mabao 19.
Katika msimu uliopita, Msuva alifanikiwa kutwaa tuzo ya ufungaji bora baada ya kuifungia timu yake jumla ya mabao 17 akifuatiwa na Tambwe aliyetikisa nyavu mara 15.

Azam macho yote kwa Prisons kesho

NA SALMA MPELI
UONGOZI wa timu ya Azam FC umesema kuwa kwa sasa macho yao yote yapo kwa Tanzania Prisons ambao wanatarajia kukutana nao kesho ikiwa ni mechi ya Kombe la Shirikisho (FA) mchezo utakaopigwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.

Akizungumza na DIMBA, Ofisa Habari wa Azam, Jafari Idd, alisema hiyo ndiyo mechi iliyoko mbele yao kwa sasa kabla ya ile ya ligi dhidi ya Toto African ya Mwanza, Aprili 3 kabla ya kukutana na Esperance ya Tunisia kwenye Kombe la Shirikisho.
“Tunajiandaa kuhakikisha tunaibuka na ushindi ili kuingia hatua ya nusu fainali, tunashukuru kikosi chetu kimekamilika baada ya wachezaji wa timu ya Taifa kurejea na kujiunga kambini pamoja na wenzao,” alisema Jaffer.
Katika msimamo wa Ligi Kuu Azam wapo nafasi ya tatu wakiwa na pointi 50 sawa na Yanga huku zikitofautiana idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa.

African Sports kusaka kocha Zanzibar

NA SALMA MPELI
UONGOZI wa African Sports ya Tanga upo katika harakati ya kumsaka kocha kutoka visiwani Zanzibar atakayeziba nafasi ya Ramadhan Aluko aliyefukuzwa hivi karibuni.
Akizungumza na DIMBA, Makamu Mwenyekiti wa timu hiyo, Abdul Bosnia, alisema wanahitaji kocha kwa haraka na tayari wapo katika mchakato huo kwa ajili ya kuanza kazi mapema ili kuinusuru timu kutoka kwenye hatari ya kushuka daraja.
“Tunahitaji kocha kwa haraka baada ya kuamua kuachana na Aluko, tumelenga kutafuta mwalimu kutoka Unguja ili aanze kazi mapema,” alisema.
African Sports ipo nafasi ya 15 kwenye msimamo wa ligi hiyo ikiwa na jumla ya pointi 20 juu ya ndugu zao Coastal Union ambao wanaburuza mkia wakiwa na pointi 19 ambapo timu hizo zote zipo kwenye hatari ya kushuka daraja.
Timu hiyo ilipanda daraja msimu uliopita na kuanza kucheza Ligi Kuu msimu huu baada ya kucheza ligi hiyo kwa mara ya mwisho mwaka 1988, lakini hata hivyo mashabiki wao wana wasiwasi mkubwa kutokana na majaliwa na timu hiyo katika msimu ujao wa ligi kwani huenda isiwepo msimu ujao.


Manara: Al Ahly iifunge Yanga 5-0

NA EZEKIEL TENDWA
UNAKUMBUKA yale mabao 5-0 ambayo Simba waliwafunga Yanga msimu wa 2012? Sasa ni hivi, msemaji wa Wanamsimbazi hao, Haji Manara, amesema anataka Al Ahly iibuke na ushindi kama huo dhidi ya Wanajangwani hao Jumamosi ya Aprili 9.
Unajua kwanini Manara ameamua kutamka maneno hayo? Jibu ni jepesi tu kwamba kama Yanga wataibuka na ushindi dhidi ya Al Ahly katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jiji halitakalika.
“Nataka Yanga ifungwe mabao 5-0 kama tuliowafunga sisi mwaka 2012 kwani hawa Yanga wakishinda mji hautakalika. Nadhani ikiwa hivi mambo yatakuwa sawa sawa na mji utakalika na kahawa itanyweka,” alisema Manara mtoto wa nyota wa zamani wa Yanga, Sunday Mnara ‘Computer’.
Yanga na Al Ahly zinatarajiwa kukutana Aprili 9 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, mchezo wa mabingwa barani Afrika.

Kiungo Simba aitahadharisha Yanga


NA ZAINAB IDDY
KIUNGO wa zamani wa Simba, Pierre Kwizera, amesikia kuwa Yanga watakabiliana na Al Ahly ya Misri katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na sasa ameamua kuwapa somo kwamba wanatakiwa waingie kwa tahadhari kubwa.
Kwizera ambaye kwa sasa anakipiga katika Klabu ya Rayon Sports ya nchini Rwanda, amesema kama kweli Yanga wana nia ya kufanya vizuri dhidi ya Al Ahly ni lazima wajipange kisawasawa kukabiliana na mbinu chafu za ndani na nje ya uwanja.
“Ukikutana na timu za Kiarabu unatakiwa uwe fiti kuanzia akili kwani jamaa wanajua kutumia viwanja vyao vya nyumbani tofauti na ukanda wetu wa Afrika Mashariki na Kati.
“Kama kweli Yanga wana nia ya kuwatoa lazima wahakikishe wanaibuka na ushindi usiopungua angalau mabao 4-0, kwani vinginevyo itawawia vigumu watakapokwenda Misri wakiwa ugenini,” alisema Kwizera.
Mchezo wa Yanga dhidi ya Al Ahly unatarajia kuchezwa Aprili 9 mwaka huu katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, huku ule wa marudiano ukitaraji kuchezwa Aprili 19 nchini Misri.

Friday, March 4, 2016

TANGAZO LA KAZI

KAMPUNI ya Wazalendo Bright Media   inatangaza nafasi ya kazi ya afisa masoko kwa  Watanzania wote.

Sifa:
1. Awe ni Mtanzania
2. Umri miaka 20-40
3. Awe na elimu ya masuala ya biashara kwa    kiwango cha Diploma kutoka  chuo               kinachotambulika.
4. Awe na uzoefu wa miaka mitatu kwa kazi anayoomba.
5. Awe na uwezo wa kuzungumza lugha ya Kiswahili na Kiingereza, anayejua lugha ya     Kifaransa, Kiarabu     itakuwa ni sifa za ziada.
6. Asifanye kazi kwa kusukumwa na awe mbunifu.
7. Awe tayari kufanya kazi popote ndani ya  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kulingana na atakavyopangiwa na mkuu wake wa kazi.

Barua zote zitumwe kwa:
Afisa Mtendaji Mkuu,
Wazalendo Bright Media,
Dar es Salaam,
Tanzania.
Barua zitumwe kwa njia ya Email:
mchakarikajitv@gmail.com
nellymtanzania@gmail.com